GATTUSO ASEMA KAMWE HAWEZI KUJIFANANISHA NA ARSENE WENGER


Kuelekea mechi yao itakayochezwa Alhamisi usiku, Gatuso akasema licha ya matumani ya kufanya vizuri lakini anaheshimu uwezo mkuwa wa kocha wa Arsenal - Arsene Wenger.


Gatuso akasema akijilinganisha na Wenger anajiona kama yupo kwenye timu ya watoto.

"Wenger ni kocha mwenye uzoefu mkubwa, amekuwa kocha kwa zaidi ya miaka 35, amekuwa Arsenal kwa zaidi ya miaka 20 lakini mimi ndiyo kwanza naanza safari yangu ambayo mbele ina kiza kingi," anaeleza Gattuso.

"Yeye anaelekea  ukingoni kwenye ukocha wake wakati mimi ndio naanza. Siwezi kabisa kujifananisha na Wenger," aliongeza Gatuso.

Pamoja na hayo, Gattuso amesema anategemea timu yake itafanya vizuri dhidi ya Arsenal katika mchezo huo wa kusaka robo fainali ya Europa League.

Labels: