PICHA 36: JAHAZI, YAH TMK, WAKALI WAO WALIVYOCHUANA JUMAPILI USIKU TRAVERTINE HOTEL


Bendi tatu za taarab Jahazi Modern Taarab, Yah TMK na Wakali Wao Jumapili usiku zilichuana vikali kwenye ukumbi wa Travertine Hotel, Magomeni, jijini Dar es Salaam.

Hakuna bendi iliyokubali kuwa ‘mnyonge’ kwani kila moja ilihakikisha inaweka silaha zake za maangamizi kwa kuchagua nyimbo zinazokubalika zaidi.

Bendi hizo zilichuana kwa mfumo wa kupokezana ambapo kila bendi ilirudi jukwaani mara mbili.

Wakali Wao iliyokuwa chini ya mtunzi na mtengenezaji mahiri wa muziki, Thabit Abdul, ndio iliyokufungua pazia la burudani katika kila mzunguko.

TMK inayojengwa na wapiga vyombo tishio, yenyewe ilikuwa ya pili katika kila mzunguko huku Jahazi inayobebwa na utajiri wa nyimbo zenye kukubalika na kufahamika zaidi ndiyo iliyokuwa ihitimisha mpambano huo.

Wakati Jahazi nyimbo zao zote zilitesa katika kila mzunguko, bendi nyingine zilitesa kwa baadhi nyimbo.

Mwitikio wa mashabiki ulikuwa ni mzuri na wa kuridhisha kulingana na hali ya uchumi kwa sasa.
 Aisha Mtamu Kabisa wa Wakali Wao akiimba "Thamani ya Pendo"
 Aisha Vuvuzela wa Yah TMK  akiimba wimbo "Kibaya Kina Wenyewe" ambao ulikubalika sana
Amina Mnyalu wa Yah TMK
 Fatma Mcharuko mmoja wa waimbaji waliotikisa Travertine
 Hadija Mbegu wa Jahazi
 Jumanne Ulaya kwenye mpini wa solo wa Jahazi
 Mwasiti Kitoronto wa Jahazi
 Rahma Machupa wa Wakali Wao na wimbo wake "Yataka Moyo"
 Mariam BSS wa Jahazi akiimba "Nipe Stara"
 Mohamed Mauji akicharaza solo la Yah TMK
 Mauwa Teggo wa Yah TMK
 Mwasiti alikuwa MC kwa upande wa Jahazi
 Fatma Mcharuko akitesa na "Siwaguni Siwakohoi"
 Miriam Amour wa Wakali Wao
 Miriam Amour
 Mishi Zele wa Jahazi akiimba "Nia Safi Hairogwi", namba nyingine iliyotikisa Travertine
 Mishi Zele akiimba kwa kujiamini
 Aisha Mtamu Kabisa wa Wakali Wao mmoja wa waimbaji waliofanya vizuri
 Mwimbaji Mohamed Ali "Mtoto Pori" wa Wakali Wao
 Mtoto Pori
 Fatma Mcharuko wa TMK akimtunza Mwasiti Kitoronto wa Jahazi
 Hali ilivyokuwa Jumapili usiku
 Omar Teggo akiimba "Figisu Figisu"
 Omar Teggo kutoka Yah TMK
 Amigo wa Jahazi katika ubora wake
 Rahma Machupa wa Wakali Wao
 Muddy K (kushoto) na Said Fella
 Thabit Abdul akipapasa kinanda cha Wakali Wao
 Prince Amigo wa Jahazi
 Umati uliofurika Travertine
 Aisha Vuvuzela wa Yah TMK
 Wadau wakifuatilia onyesho kwa makini
 Waimbaji wa Jahazi
 Hadija Mbegu wa Jahazu akisepa na kijiji
Waimbaji wa Wakali Wao


Labels: